.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 29 Oktoba 2017

ANTHONY MARTIAL ATOKEA BENCHI NA KUIPA MAN U USHINDI

Goli la ushindi lililofungwa katika dakika za mwisho na Anthony Martial, limeendelea kuiweka Manchester United katika nafasi ya pili ya Ligi Kuu ya Uingereza wakati wakiifunga Tottenham katika dimba la Old Trafford.

Kuingizwa kwa Martial katika dakika ya 70 kuchukua nafasi ya Marcus Rashford hakukuwafurahisha mashabiki wa Manchester United, lakini kocha Jose Mourinho alionekana alikuwa sahihi baada ya kufunga goli.
  Mshambuliaji Mfaransa Anthony Martial akiifungia Man Utd  goli pekee katika mchezo huo
Katika mchezo mwingine Leroy Sane amewasaidia vinara wa Ligi Kuu ya Uingereza kuibuka na ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya West Brom, lakini kocha Pep Guardiola amewaona wachezaji wake kuwa wanapaswa kuwa makini katika kupachika magoli.

Katika mchezo huo City walimiliki mpira kwa asilimia 78 na kutengeneza nafasi 15 za kufunga, huku David Silva akikosa nafasi mbili za kufunga magoli, wakati naye Kevin de Bruyne shuti lake likilenga nyavu kwa pembeni.
    Leroy Sane akifunga goli la kwanza Manchester City katika mchezo wao dhidi ya West Brom

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni